MTOTO MWENYE MIAKA 03 AUWAWA KIFO CHA UTATA KATAVI,WAZAZI WAKAA NA MAITI NDANI YA NYUMBA KWA SIKU 4,MAJIRANI WARIPOTI TUKIO POLISI BAADA YA KUKERWA NA HARUFU MBAYA


Na.Issack Gerald-Mpanda Katavi
WATU wawili ambao ni wazazi wa mtoto aliyefahamika kwa jina la Justina Laurent (3) wanashikiliwa na jeshi la polisi Mkoani Katavi kwa kusababisha kifo cha mtoto huyo ambaye aligundulika akiwa amefariki dunia ndani ya chumba cha wazazi wake huku akiwa na majeraha sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kamanda msaidizi wa Jeshi la Polisi Mkoani Katavi ACP Rashid Mohamed amesema kuwa tukio hilo limetokea jana Februari 24 katika mtaa wa Mji wa Zamani Kata ya Kashaulili Wilayani Mpanda.
ACP Mohamed amewataja wazazi hao kuwa ni Mariam Elias (20) na Juma Suleiman (24) wote wakazi wa mtaa wa Mji wa Zamani.
Aidha Kamanda Mohamed amesema kuwa Mwili wa marehemu umeonekana ukiwa na majeraha sehemu za kichwani, miguuni, mbavuni, tumboni na mikononi majeraha ambayo yanatiliwa shaka huenda yakawa ya kuunguzwa na moto ama ugonjwa wa ngozi.
Katika mahojiano ya awali na wazazi wa mtoto huyo walikiri kwamba marehemu alianza kuugua ugonjwa wa ngozi tangu tarehe 18.02.2016 lakini hawakuwahi kumpeleka hospitali
Hata hivyo Mpaka sasa chanzo cha majeraha hayo yaliyosababisha kifo chake bado kujulikana.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ametoa wito kwa wananchi kuwa na kawaida ya kutoa taarifa yoyote inayotiliwa shaka kwenye vyombo vya dola ili hatua ziweze kuchukuliwa kwa haraka na kwa wakati lakini pia ameiasa jamii kuacha kushiriki kufanya vitendo vya kishirikina.
Kwa upande wa majirani wa familia hiyo wamesema kuwa mwili wa marehemu umekuwa ndani ya nyumba kwa siku ya nne hadi leo tangu kuuwawa kwa mtoto huyo na harufu mbaya iliyokuwa ikitoka ndani ya nyumba ya watuhumiwa ndiyo imepelekea kupeleka taarifa polisi na hatimaye upekuzi kufanyika na kugundua mwili huo.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA