WAWILI WAFIKISHWA MAHAKAMANI MPANDA,MMOJA KUTISHIA KUUWA KWA MANENO MWINGINE KUUZA KIWANJA KWA ZAIDI YA MTU MMOJA


Na.Issack Gerald-Mpanda
MTU mmoja amefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda jana, akikabiliwa na shtaka la kuuza kiwanja kwa gharama ya shilingi laki sita na baadaye kukiuza kwa mtu mwingine.

Imeelezwa mahakamni hapo kuwa, mshtakiwa Shukuru Salum alitenda kosa hilo tarehe nane mwezi Juni mwaka 2015 katika eneo la Nsemulwa mjini Mpanda kwa kumuuzia Bi Aziza kiwanja na hatimaye kukuiuza kwa mtu mwingine ambaye tayari ameshajenga katika kiwanja hicho.
Akitoa ushahidi mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Robert Nyando, malamikaji amesema mshtakiwa aliahidi kurejesha fedha hizo lakini hadi sasa hajatekeleza.
Hakimu Nyando amesema mahakama imeona mshtakiwa ana kesi ya kujibu na kumtaka ajitetee. Mshtakiwa katika utetezi wake amesema ana mashahidi wawili ambao ameamuriwa na mahakama kuwapeleka mahakamani hapo tarehe 1 mwezi Februari mwaka huu, kesi hiyo itakaposikilizwa kwa ajili ya utetezi.
Wakati huo huo,mtu mmoja amefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda, akikabiliwa na shtaka la kutishia kuua kwa maneno.
Akisoma shtaka hilo mbele ya hakimu Robert Nyando, Koplo Fulgenzce wa jeshi la polisi Mpanda amemtaja mshtakiwa kuwa ni Noel Katobasho (76) na alitenda kosa hilo tarehe tano mwezi huu katika kijiji cha Uruwila na aliwatishia kuwaua walalamikaji Pascalia Makamba na Gaudence Katobasho, kuwa wakiendelea kulima katika mashamba anayodai ni mali yake, wataona atakachowafanyia.
Hakimu Nyando ameamuru mshtakiwa apewe dhamana ya shilingi laki mbili na mdhamini awe na kitambulisho, na kuagiza katika kesi hiyo abaki mlalamikaji mmoja na mwingine awe shahidi, polisi ibadili hati ya mashtaka baada ya kubainika ana shtaka la pili.
Kesi hiyo itatajwa tena terehe mbili mwezi Februari mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA