MKUU WA MKOA WA KATAVI ATAKA KILA MKAZI KUWA MLINZI WA MAZINGIRA YANAYOMZUNGUKA


Na.Issack Gerald-Mpanda
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dk.Ibrahim Msengi,amemtaka kila wakazi wa Mkoa wa Katavi kuwa mlinzi wa mazingira yanayomzunguka.

Wito huo umetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wakati wa uzinduzi siku ya wa upandaji miti kimkoa ambao umefanyika katika katika Halmashauri ya  wilaya ya  Nsimbo, kata ya kanoge kijiji cha Kanoge  kitongoji cha barabara ya pili-Kanoge.
Aidha Dk.Msengi amesema kuwa suala la upandaji miti lisiishie kuonekana katika takwimu za maandishi na badala yake wahakikishe misitu iliyopandwa inaonekana.
Wakati huo huo amewataka venyeviti wa vijiji na kila muhusika kuhakikisha hakuna mfugaji anaye hamia bila kufuata utaratibu.
Hata hivyo,Dk Msengi ametaka uandaliwe utaratibu kukabidhiana na kusimamia  mashamba ya miti na ukaguzi uwe unafanyika kila  baada ya miezi mitatu kulingana na ratiba itakavyoelekeza ili ikitokea miti imekufa ijulikane nani wa kutoa taarifa na sababu ya miti kufa.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA