TUME YA ARDHI MPANDA YATOA TAARIFA YA UCHUNGUZI MIGOGORO YA ARDHI KWA BAADHI YA VIJIJI



Na.Issack Gerald-Mpanda
TUME ya uchunguzi wa migogoro ya ardhi imetoa taarifa baada ya kufanya uchunguzi katika vijiji vya Ikaka, Nkungu na Kapalamsenga wilayani Mpanda.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu maazimio yaliyofikiwa baada ya kupokea taarifa hiyo, Mkuu wa wilaya ya Mpanda Bw. Paza Mwamlima amesema miongoni mwa maazimio ni pamoja na halmashauri ya wilaya ya Mpanda kuwa na utaratibu wa kupima ardhi katika vijiji na iwe inatoa ushauri wa kitaalam kwenye kamati za ardhi za vijiji.  
Aidha, amemuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mpanda kupitia idara ya ardhi na maliasili afungue mashtaka, baada ya uongozi wa kijiji cha Kapalamsenga, uliokuwepo kukiuka sheria ya wanyamapori na kuuza eneo la Lyamgoloka kwa wananchi 52 mwaka 2013.
 Maeneo hayo ni miongoni mwa maeneo mengi yenye migogoro ya ardhi Mkoani Katavi ambapo mogogoro mingi wamekuwa wakilalamikiwa idara ya ardhi kwa kupima kiwanja kwa zaidi ya mtu mmoja.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA