ASKARI 15 KATAVI WATUNUKIWA VYETI VYA HESHIMA POLICE FAMILY DAY,WAPANGA MIKAKATI YA KUKOMESHA UHARIFU



Na.Lutakilwa-Lutobeka-Katavi
MAAFISA 15 wa jeshi la polisi mkoani Katavi wametunukiwa vyeti maalum vya utendaji kazi katika maadhimisho ya siku ya polisi yaliyofanyika leo mjini Mpanda.

Akitunuku vyeti hivyo Kamishna msaidizi wa jeshi la polisi  kamanda Dhahiri Kidavashali amesema kutokana na kazi kubwa waliyofanya maafisa hao, kubaini matukio mbalimbali ya kiuharifu ni bora wakawapa vyeti hivyo kama motisha.
Mbali na kutunuku vyeti kamanda Kidavashali ametumia sherehe hizo kama sehemu ya kutathmini kazi zilizofanywa na jeshi kwa mwaka mzima wa 2015 ili kubaini mafanikio na mapungufu.
Wananchi waliohudhuria sherehe hizo wameelezea kufurahishwa na utendaji kazi wa jeshi la polisi kwa mwaka 2015, kwani askari wamekuwa marafiki wa wananchi.
Sherehe hizo za POLICE DAY ambazo zimefanyika katika viwanja vya polisi Wilayani Mpanda, zilihusisha michezo mbalimbali ikiwemo riadha na kucheza ngoma.
Hata hivyo Mkoani Katavi,kumekithiri matatizo ya watu kuuwawa mara kadhaa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Katavi ambapo watu hawa huuwawa na watu wasiojulikana lakini pia wengine kuuwawa na wanyama wakali kama simba.
Karibu watu 10 wamepoteza maisha katika mazingira ya kutatanisha wengingi wao wakiwa ni wanaume.
Hata hivyo jeshi la polisi limesema kuwa,kupitia sherehe hizo,limewasihi wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kuwabaini waharifu kabla ya  athari kutokea kwa binadamu.
Maadhimisho siku ya polisi  mkoani katavi yamefanyika yakiwa na kauli mbiu “UTII WA SHERIA BILA SHURUTI, KATAVI BILA UHARIFU INAWEZEKANA”.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA