BREAKING NEWS : WALIMU 120 MIKOA YA RUKWA,KATAVI NA KIGOMA WAPATIWA MAFUNZO KUINU KIWANGO CHA UFAULU WA WANAFUNZI


Na.Issack Gerald-MPANDA
JUMLA ya Walimu  120 wa Shule za msingi kutoka halmashauri 8 za  Mikoa ya Rukwa, Kigoma na Katavi wanashiriki mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu na wanafunzi katika ufundishaji na ujifunzaji ili kuboresha taaluma na kuongeza kiwango cha  Ufaulu kitaifa.

Akifungua Mafunzo hayo katika Shule ya Sekondari Mwangaza Manispaa ya Mpanda Mgeni rasmi, Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Katavi Said Mwapongo, amewataka walimu walioshiriki mafunzo kuhakikisha wanawajengea uwezo walimu wenzao ambao hawakushiriki mafunzo hayo.
Mafunzo hayo yanalenga walimu wa masomo ya Kiswahili, kingereza na hisabati, ikiwa Sehemu ya mpango wa Matokeo makubwa sasa (BRN), yalioandaliwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, na yameanza  Januari 4 na yatamalizika Januari 8 mwaka huu.
Baadhi ya wajumbe wa semina hiyo wamesema kuwa,walimu hao kupatiwa mafunzo hayo kutaongeza ufanisi katika kutekeleza haraka mpango wa Mtokeo Makubwa sasa na kupunguza idadi ya wanafunzi wanaoshinwa kufaulu mithani kwa kiwango kikubwa.
Hivi karibuni Wakati Mkoa wa Katavi ukishika nafasi ya kwanza kitaifa katika matokeo ya darasa la saba,Mkoa jirani wa Rukwa kwa mjibu wa Mkuu wa Mkoa wa mkoa huo Magalula Said Magalula,amesema mkoa huo umeshika nafasi ya tatu kutoka mwisho katika shule za msingoi zilizofanya mtihani wa darasa la saba kwa mwaka 2015.
Endelea kuwa na P5 TANZANIA hivi punde kwa undani wa habari hii

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA