WAZAZI NA WALEZI WATAKIWA KUTAMBUA HAKI ZA MTOTO KUZUIA UKATIRI


Na.Agness Mnubi-MPANDA.
WAZAZI na Walezi mkoani Katavi wametakiwa kutambua umhimu wa haki za watoto na kuepuka Mazingira yanayopelekea ukatili na unyanyasaji kwa watoto hao.

Akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA na Mpanda Rdaio Mwenyekiti wa Asasi ya Faraja na  Urafiki kwa Wanandoa na Ushauri kwa Vijana (FUNUVI ) Bi. Neema Kidima amesema Maelewano mabaya katika ndoa na kutalikia ni miongozni mwa vyanzo vinavyopelekea   kutotambua haki za watoto na kusabaisha mazingira ya ukatili na unyanayasaji.
Bi. kidima  ameomba Wadau wanaojihusisha na kupinga ukatili ,Haki za binadamu, pamoja na serikali kushirikiana kutoa elimu katika jamii juu ya haki za watoto.
Desemba 18        Mwaka huu, watoto 62 wakiwemo wawili wenye ulemavu wa ngozi (albino) walifichuliwa Wilayani Mpanda na  kamati ya baraza la watoto, wakiwa katika mazingira yanayowanyima haki zao ikiwemo kupatiwa  elimu, kwa kipindi cha mwezi Juni hadi Desemba.



Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA