WATOTO 62 WENYE MAHITAJI MAALUMU WAIBULIWA MPANDA,WAMO ALBINO WAWILI WALIOPELEKWA SUMBAWANGA KUSOMA


Na.Issack Gerald-MPANDA
Jumla ya watoto 62 wenye mahitaji maalumu wakiwemo wawili wenye ulemavu wa ngozi albino wamefichuliwa Wilayani Mpanda wakiwa katika mazingira yanayowanyima haki zao za msingi ikiwemo kupatiwa  elimu kwa kipindi cha mwezi Juni hadi Desemba mwaka huu.
                                           
Baadhi ya watoto wenye mahitaji maalumu Wilayani Mpanda.PICHA Na.Issacka Gerald

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa elimu Jumuishi Mkoani Katavi Bw.Raphael Fortunatus wakati akiwasilisha taarifa ya kamati ya elimu Jumuishi Wilayani Mpanda mbele ya mratibu wa Elimu Jumuishi katika Mikoa ya Rukwa na Katavi kupitia kikao cha kamati hiyuo ambacho kimefanyika leo katika Ofisi za kamati hiyo zilizopo Wilayani Mpanda.
Bw.Fortunatus amesema,idadi hiyo imepatikana katika kipindi cha Mwezi Juni hadi Desemba mwaka huu katika kata za Kakese mkwajuni na mbugani ambapo wamepatikana watoto19,Kawanzige watoto 28 na Mwamkuru watoto 15.
Aidha amesema kuwa walemavu wawili wa ngozi albino walioibuliwa kijiji cha kakese ni Catherine Chemuka(11) na Peter Chemuka (9) ambao wote wanaendelea na masomo katika shule ya Msingi Malangari iliyopo Wilayani Sumbawanga huku wakiishi katika bweni kujikinga na wimbi la mauji ya kikatiri dhidi yao.
Mbali na kuendelea na mikakati ya kuwaibua zaidi watoto wenye mahitaji maalumu,kamati imetoa mafunzo kwa walimu 26 Wilayani Mpanda kuwajengea uwezo wa kuwasaidia watoto wanaoibuliwa.
Katika hatua nyingine Jumatatu ijayo ya Desemba 21 mwaka huu,kamati hiyo inatarajia kumwandikia barua Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda ili kumwomba afungue madarasa ya wanafunzi wenye ulemavu wa kusika viziwi katika shule ya msingi Azimio waliozuiwa na mkandarasi aliyefunga madarasa hayo akishinikiza kulipwa pesa zake ambapo hadi sasa ni mwaka mmoja madarasa hayo hayatumiki huku kuanzia darasa la kwanza hadi la saba wakisomea katika chumba kimoja kibovu ambapo walimu watatu huingia kufundoisha kwa wakatik mmoja katika ubao mmoja.
Kwa upande wake mratibu wa elimu jumuishi katika mikoa ya Rukwa na Katavi Bw.Joseph Ndomba,ameitaka kamati hiyo kushirikiana kwa ukaribu na idara za serikali kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto wenye mahitaji maalumu.
Kamati hiyo yenye wajumbe wapatao 12,inajumuisha idara mbalimbali zikiwemo wakuu wa idara za maendeleo ya jamii katika Manispaa ya Mpanda,viongozi wa dini,wazazi na walezi wenye watoto walemavu na wasio na walemavu na Chombo cha habari cha Mpanda Radio Fm ambapo mwakilishi ni Issack Gerald mwandishi wa habari wa kituo hicho.
Wakati huo huo kupitia kikao hicho kamati imependekeza kukutana mara kwa mara kupanga mikakati ya kuibua watoto waliofichwa wenye mahitaji maalumu ili wapatiwe elimu huku wazazi wakiaswa kutoa ushirikiano na kuachana na tabia ya kuwaficha.
Kamati ya elimu jumuishi Wilayani Mpanda inafanya kazi chini ya ufadhili wa mashirika matatu yaliyoungana na kuunda umoja wao unaojulikana kama IFI.
Mashirika haya  ni International Aids Services(IAS),Free Pentekoste Church Of Tanzania(FPCT) na International Center Of Disabilities

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA