KAMATI ELIMU JUMUISHI MPANDA KUFANYA KIKAO LEO


Na.Issack Gerald-MPANDA
Kamati ya kushughulikia elumu jumuishi Wilayani Mpanda Mkoani Katavi,leo wanatarajia kukutana na wadau wa elimu hiyo kujadili masuala mbalimbali.

Akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA Mratibu wa elimu Jumuishi Mkoani Katavi Bw.Raphael Fortunatus,amesema kikao hicho kinatarajia kufanyika katika ofisi za Elimu Jumuishi zilizopo Manispaa ya Mkoani Katavi.
Licha ya kutobainisha mambo yatakayojadiliwa katika kikoa hicho,mambo ambayo yamekuwa jakijadiliwa kupitia vikao kama hivyo ni pamoja na namna ya kumwezesha mtoto aliyeko mazingira magumu kupata haki sawa kama watoto wengine hususani sekta ya elimu.
Kmati ya elimu Jumuishi Wilayani Mpanda inaundwa na idara mbalimbali zikiwemo  asasi za kidini na binafsi huku katika vyombo vya habari mwakilishi katika kamati hiyo akitokea Mpanda Radio fm.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA