JESHI LA POLISI KATAVI LAANZA KUTOA TAHADHARI MSIMU WA SIKUKUU 2015


Na.Issack Gerald-Katavi
Wakazi Katika Mkoa wa Katavi wametakiwa kuepukana na Mazingira hatarishi Katika kipindi hiki cha kuelekea Kipindi cha sikuku za Krismasi na mwaka mpya.

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa jeshi la polisi Mkoani      hapa ACP Zahir Kidashavari katika taarifa yake kwa vyombo vy habari kuhusu mikakati ya jeshi la polisi Kuimarisha usalama Katika Kipindi cha sikukuu.
 Katika taarifa yake ACP Kidavashari amesema uzoefu unaonyesha kuwa Matukio mengi ya uhalifu ikiwemo wizi na ulevi wa kupindukia hujitokeza na hivyo kuwataka wananchi wote kuchukua tahadhari.
Aidha Kamanda Kidavashari amewashukuru wananchi wote wa Mkoa wa Katavi kwa kuonesha imani na kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuhakikisha Mkoa wa Katavi unaendelea kuwa salama dhidi ya vitendo vinavyozorotesha ustawi wa amani na utulivu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA