WANUFAIKA NA TASSAF WAPONGEZA MRADI HUO WILAYANI MLELE


Na.Issack Gerald-Mlele.
BAADHI ya wakazi wa Ilunde na Isegenezya kata ya Inyonga wilayani Mlele Mkoani Katavi wameupongeza mradi wa kunusuru kaya masikini tasaf  kwa kuwawezesha kujikwamua kimaisha.

Wakizungumza na P5 TANZANIA MEDIA katika kijiji cha Ilunde wamesema mpango huo umewawezesha kusomesha watoto wao na kupata baadhi ya huduma nzuri tofauti na hapo awali ambapo mpango huo ulikuwa hauja wafikia.
Hata hivyo wameiomba serikali ya awamu ya tano kuimarisha mfuko huo wa tasaf ili kuzifikia kaya maskini katika maeneo mbalimbali katika mkoa wa katavi na mikoa mingine iliypo nchini.
Kwa upande wake mratibu wa tasaf wilayani mlele Lucas Kombe amewataka wananchi hao kutumia fedha hizo kwa malengo yanayokusudiwa na mfuko huo ili kupunguza umaskini katika kaya hizo.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA