MKUU WA MKOA WA RUKWA AAGIZA KUOANDOLEWA MAAFISA WANNE KITENGO CHA FORODHA MKOANI HUMO



Baadhi ya magogo yaliyokamatwa

Na Mwandishi wetu-SUMBAWANGA.
MKUU wa Mkoa wa Rukwa Magalula Ssaid Magula ameagiza kuondolewa mara moja kwa maofisa wa vitengo vinne kutoka katika kituo cha forodha cha Kasesya mpakani mwa nchi ya Zambia wilayani Kalambo mkoani humo kwa tuhuma za kushindwa kutekeleza maadili ya utumishi wa umma.

Mkuu huyo wa mkoa amefika kituoni hapo akiwa na ujumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kufuatia kukamatwa kwa roli la zaidi ya tani 40 lililosheheni magogo ya miti aina ya mkurungu uliopigwa marufuku kusafirishwa.
Magalula amesema, dalili zinaonesha maafisa hao wanasaidizana na wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu kuhujumu uchumi wa nchi ambapo magogo hayo thamani yake haijajulikana.
Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa ametoa wiki moja kwa Ofisa Upelelezi Mkoani Rukwa (RCO) kukamilisha uchunguzi wa tukio hilo na kumkabidhi matokeo yake.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA