VIKUNDI VYA ULINZI VYAMA VYA SIASA VYAPIGWA MARUFUKU


Na.Issack Gerald-KATAVI
Jeshi la Polisi Mkoani Katavi limevitaka vyama vya siasa na wafuasi wao kuzingatia kanuni,sheria na taratibu za vyama vyao kudumisha amani ya nchi na kuepuka makosa ya jinai yanayoweza kuwatia hatiani.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mratibu mwanadamizi wa Jeshi la Polisi Mkoani Katavi Focus Malengo wakati wa Mahojiano Maalum na P5 TANZANIA.
Aidha Malengo amewataka viongozi wa vyama vya siasa,wafuasi wao na wamiliki wa vyombo vya usafiri kutotumia magari yasiyoruhusiwa kisheria ili kuepuka uvunjifu wa sheria za barabarani na hatimaye kuzuia ajali zisizo za lazima.
 Wito huo wa jeshi la polisi unatolewa ikiwa ni siku ya tano tangu kampeni za uchaguzi Mkuu kuzinduliwa kwa mjibu wa Katiba ya nchi ambapo uchaguzi unatarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA