BARABARA YA MPANDA-TABORA SASA RUKSA KWA MAGARI YOTE


Mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Mhuga hatimaye ametangaza rasmi kuwa magari yote makubwa kwa madogo yanaruhusiwa kusafiri kwa kutumia barabara ya Mpanda --Tabora kupitia Mto Koga wilayani Mlele Mei 30,2018.
Kwa mjibu wa Bw.Aman  Mwakalebela ambaye ni Afisa Mfawidhi wa mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa majini na nchi kavu SUMTRA amesema hali ya barabara hiyo ni nzuri na inaruhusu magari ya aina zote kupita.
Hata hivyo Mwakalebela amewataka abiria waliotoa nauli ya mzunguko wa barabara kupitia Kigoma au Mbeya kwa ajili ya kwenda Tabora kudai kurejeshewa kiasi cha  nauli iliyozidi kiwango cha fedha kutoka Mpanda-Tabora na kusafiri kwa gharama halisi.
Mei 26 mwaka huu Mkuu wa mkoa wa katavi Meja Jenerali Mstaafu Rapahael Muhuga alitangaza kuruhusu magari yasiyozidi tani 3 huku ukarabati wa barabara hiyo ukiendelea.
Aprili 14 mwaka huu,Muhuga alitanagaza kuifunga barabara hiyo kutokana na kujaa maji katika daraja la mto koga hali iliyokuwa ikihatarisha usalama wa watumiaji wa barabara.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA