MKE WA ZAMANI WA NELSON MANDELA AFARIKI DUNIA-FAHAMU HISTORIA YAKE


WINNIE MANDELA,mke wa zamani wa Nelson Mandela, ambaye pia alipigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini amefariki dunia akiwa na miaka 81. Habari za kifo chake zimethibitishwa na msaidizi wake.
Winnie alizaliwa mnamo 26 Oktoba mwaka 1936,na ingawa yeye na mumewe - Nelson Mandela - walitalikiana mapema miaka ya 1990,Winnie Madikizela Mandela kama alivyofahamika rasmi alisalia kutoa mchango katika maisha ya Bw.Mandela.
Msemaji wa familia Victor Dlamini amesema kupitia taarifa kuwa:"Amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu, ambapo amekuwa akiingia na kutoka hospitalini mara kwa mara tangu mwanzo wa mwaka na alifariki mapema leo Jumatatu adhuhuri akiwa amezungukwa na familia na wapendwa wake."
Kwa mjibu wa shirika la habari la AFP Askofu mstaafu na mshindi wa tuzo ya Nobel Desmond Tutu amemsifu kama "ishara kuu ya vita dhidi ya ubaguzi wa rangi ambapo Winnie alikuwa na miaka 20 hivi akiwa katika siasa.
Alisomea kazi ya utoaji huduma za kijamii na haraka aliyazoea maisha ya kuwa mama na mwanasiasa.
Katika kipindi chote cha miaka 27 mumewe alipokuwa gerezani bila matumaini ya kuachiwa huru kutokana na hukumu ya kifungo cha maisha jela alichopewa mwaka 1964,Bi Winnie alilazimika kubeba jukumu la ulezi wa watoto na pia kuendeleza kampeni za kisiasa kutaka mashujaa wa kupigania nchi yao waachiwe huru hasa mumewe.
Kutokana na hayo Bi.Winnie Mandela alilazimishwa kusalia tu huko Brandford katika jimbo lao la Orange Free katika miaka ya 70 baada ya operesheni mojawapo za kupambana na ubaguzi wa rangi zilizokuja kujulikana zaidi kama the Soweto Uprising.
Bi.Mandela mwaka 1988 alihusika makubwa kukabiliana na utawala wa ubaguzi wa rangi.
Kama ilivyomtokea mumewe, Bi Winnie alifungwa gerezani,na hata kuwekwa katika kizuizi cha pekee yake ambacho ni mojawapo ya vifungo vigumu zaidi gerezani vinavyowaathiri wafungwa kisaikolojia.
Lakini baada ya kuachiwa kwake mtindo wa mapambano yake dhidi ya ubaguzi wa rangi ulianza kupata sifa mbaya hasa pale alipoonekana kuendekeza tabia ya kuwavisha tairi shingoni wale waliolengwa kwa tuhuma za usaliti na kisha kuwachoma moto.
Walipatikana kuhusika katika kitendo cha kumteka nyara na kumuua kijana mmoja mwenye umri wa miaka 14 aitwae Stompie Moeketsi -kwa tuhuma za kwamba alikuwa akitoa siri kwa maadui zao.
Japo Bi.Winnie Mandela aliepuka hukumu ya kifungo jela - baadaye tume ya ukweli na maridhiano iliyoongozwa na askofu Desmond Tutu,iliyokuwa inachunguza ukweli kuhusu matendo tata katika vita dhidi ya ubaguzi wa rangi na kutafuta maridhiano,ilimpata Bi Mandela na hatia ya kutowajibika kisiasa wala kimaadili wakati wa kitendo hicho.
Licha ya misukosuko hiyo Bi.Mandela alibaki kuwa mtu muhimu sana katika siasa za Afrika kusini na kuwa mwakilishi muhimu wa wanawake waliopambana kufa na kupona dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi uliokuwa unaendelezwa na Wazungu walio wachache nchini humo.
Katika siku za baada ya uhuru wa Afrika Kusini anakumbukwa zaidi kwa kuwa miongoni mwa wachache katika uongozi wa ANC waliomuunga mkono aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Thabo mbeki katika kushtumu na kulaani vikali vitendo vya kuwashambulia wahamiaji wa Kiafrika huko nchini Afrika Kusini.
Pia amekuwa muungaji mkono mkubwa wa kiongozi wa chama cha Economic Freedom Fighters CHA Julius Malema,kilichojimegua kutoka ANC ambacho kilimkosoa vikali rais aliyelazimika kung'atuka Jacob Zuma.
Historia ya Bi.Winnie Madikizela Mandela,hadi kifo chake inabaki akikumbukwa zaidi kama mama wa taifa la Afrika kusini aliyesimama kidete dhidi ya ubaguzi wa rangi katika umri wake wote.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA