MUFTI ZUBERI AFUNGA MKTANO MKUU WA BAKWATA AWAASA WAISLAMU KUBADILIKA


Mufti Mkuu wa Tanzania,Sheikh Abubakar Zuberi, amesema wakati umefika kwa Baraza Kuu la Waislaam Tanzania,BAKWATA kubadilika ili kuendesha shughuli zake kiuweledi na kuachana na kufanya kazi kwa mazoea.
Mufti Zuberi ametoa rai hiyo Mjini Dodoma leo wakati akifunga mkutano mkuu wa siku mbili wa Bakwata.
Amesisitiza haja ya baraza hilo kuelekeza nguvu zake katika kuwahudumia waumini wa dini ya Kiislaam nchini ambapo amesema kufanya kazi katika mtindo huo kunalenga kuwaunganisha Waislaam.
Kwa upande wake,Mkurugenzi wa Elimu wa Bakwata, Sheikh Ali Abdallah Ali amesema,mkutano huo umewasilisha mapndekezo ya maazimio 32 kwa lengo la kulijenga baraza hilo.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA