DC AAGIZA WALIOKAIDI KUFANYA USAFI WAKAMTWE


Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Bi.Lilian Matinga ameagiza kuchukuliwa hatua kwa wafanyabiasha wa soko la Buzogwe katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda baada ya kukaidi agizo la kufanya usafi katika maeneo ya soko hilo.
DC Lilian Matinga Picha na Issack Gerald
Matinga ametoa agizo hilo leo wakati akishiriki zoezi la usafi katika soko la Buzogwe akiwa ameambatana na maafisa wa jeshi la polisi pamoja na watumishi wakiwemo watumishi wa umma.
Amesema kuwa katika soko hilo hakuna aliyefanya usafi zadi ya mwenyekiti wa soko ambapo amesema watakaochukuliwa hatua watawajibishwa kwa kulipa faini ya shilingi 50,000 ikiwezekana hata kupelekwa mahabusu.
Baadhi ya wananchi ambao wameshiriki zoezi la usafi wamesema kama serikali itaendelea kuhamasisha usafi mara kwa mara hakutakuwa na hofu ya magonjwa ya mlipuko.
Jana mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga,aliagiza watumishi wa umma na wananchi kushiriki katika zoezi la usafi kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 46 ya kifo cha Rais wa kwanza wa Zanzibar  Hayati Sheikh Abeid Amani Karume aliyefariki dunia Aprili 7 mwaka 1972 kwa kupigwa risasi hadharani wakati akicheza bao.
Habari zaidio ni www.p5tanzania.blogspot.com 

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA