TANZANIA YARIDHIA KUFUTA TOZO YA DOLA ZA KIMAREKANI

Tanzania imeridhia kufuta tozo ya Dola za Kimarekani 40 inayotozwa kwa kila stika katika magari yanayosafirisha mizigo kwenda nje ya nchi.

Hatua hii imefikiwa katika Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara,Viwanda,Fedha na Uwekezaji la Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao umeafnyika Jijini Arusha
Akizungumza katika Mkutano huo,Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles Mwijage amesema Tanzania imefikia hatua hii ikiwa ni moja ya jitihada za kuendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini na Jumuiya kwa ujumla.
Tozo hii imekuwa ikitozwa kwa kipindi cha muda mrefu kwa malori yanoyosafirisha mizigo kwenda sehemu mbalimbali nje ya mipaka ya nchi.
Mkutano huu uliofanyika Februari 7 mpaka 9 mwaka huu pamoja na mambo mengine ulilenga kujadili na kutatua vikwazo vya kibiashara visivyo vya kiushuru ambavyo vimekuwepo kwa muda mrefu katika Jumuiya.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA