MPANDA RADIO YAONGOZA WANANCHI KATAVI KUSHEREHEKEA VALENTINE DAY KWA KUCHANGIA DAMU SALAMA
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani
Katavi Mh.Salehe Mbwana Muhando,amekipongeza kituo cha matangazo cha Mpanda
Radio kwa kuadhimisha siku ya wapendanao kwa kuwaunganisha Watanzania kwa
kuchangia damu salama ili kunusuru wagonjwa.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa
Mpanda Radio Bi.Salome Mchawa,amesema Mpanda Radio kama radio ya kijamii
itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kujali mahitaji ya jamii huku akiwashukuru
na kupongeza watanzania kwa kuunga mkono kampeni ya uchangiaji damu salama iliyoanzishwa
na Mpanda Radio kama kushrehekea siku ya wapendanao’’Valentine Day’’.
Kituo cha Matangazo cha Mpanda Radio
Fm kilichoanzishwa mwaka 2013 na kuzinduliwa na mwenge wa uhuru Julai 17,2013
kimeendesha zoezi la kuchangia damu salama huku kauli mbiyu ikisema‘’Changia Damu salama Okoa Maisha’’.
Kampeni hii iliyoanza kuwahamasisha
wananchi tangu mwezi uliopita imewahusha viongozi wa kiserikali,vyama vya siasa,
mashirika ya kiserikali na kiraia pamoja Wanakatavi .
Siku ya wapendanao maarufu ‘’Valentine
Day’’ ni siku ya Kumkumbuka Padre aliyeitwa Mtakatifu Valentine aliyeuwawa na warumi akipinga watu kufanya ngono
bila kuoa.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED
Comments