UJENZI WA VYOO VYA SOKO KUANZA NSIMBO,MWENYEKITI WA HALAMSHAURI AONYA

Ujenzi wa vyoo katika soko la Mnyaki kata ya Katumba Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi,unatarajiwa kuanza kesho baada ya muda mrefu eneo hilo kukosa vyoo.

Mwenyekiti wa soko la hilo Leonard Kigwasu amesema  ujenzi huo unaanza kutokana na kukamilika zoezi la ukusanyaji wa fedha.

Aidha Kigwasu ameiomba Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo kusaidia upatikanaji wa huduma ya maji katika soko hilo ili kuboresha hali ya usafi.

Kauli hiyo inapingana na Kauli aliyoitoa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya nsimbo Rafael Kalinga ambaye amekanusha uwepo wa mchango wa ujenzi wa vyoo na kuahidi kufanya uchunguzi wa jambo hilo na kuchukua hatua endapo kutakuwa na ukiukwaji wa taratibu.


Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA