TAARIFA YA SERIKALI KUHUSU KUZIMWA KWA 'CHANELI' ZA BURE KWENYE VING'AMUZI

Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbas amesema, kwa mujibu wa sheria iliyopo sasa vituo vyote vya runinga ambavyo vimepewa leseni ya FTA (Free to Air) vinapaswa kuonekana hata baada ya kifurushi kwenye kisimbusi kwisha.
Dkt.Hassan Abbas
Ufafanuzi huu unatolewa kufuatia uwepo wa malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa wananchi kuhusu kukosa huduma ya runinga za bure pindi vifurushi katika visimbusi (ving’amuzi) vyao vinapomalizika
Dkt.Abbas amesema hadi sasa kuna vituo 16 vya runinga vya ndani ya nchi vilivyopewa leseni hizo vikiwemo vituo vya ITV,Clouds TV na Channel 10.
Amesema ili mtumiaji atazame Runinga hata baada ya kufurushi chake cha malipo kwisha,kituo cha runinga (mfano ITV) kinapaswa kuwalipa warushaji wa masafa (mfano Azam) ili ITV iweze kuonekana kwa wananchi hata ambao hawajalipia visimbusi vyao.
Wakati huo huo Dkt.Abbas ametahadharisha kuwa, endapo kituo cha runinga hakitawalipa wasafirishaji wa masafa watakatiwa huduma na hivyo kuwafanya wananchi washindwe kutazama runinga bure.
Kuhusu TBC kuonekana katika visimbusi vyote hata bila malipo,msemaji amesema kila kisimbusi kinatakiwa kuweka TBC kupitia sera ya ‘must carry’ ambayo inaiwezesha kuonekana kwa wananchi bila malipo yoyote.
Kwa sasa serikali haina mfumo wa kuwaadhibu wamiliki wa vituo vya runinga wenye leseni za FTA lakini hawawalipi warusha masafa ili wananchi watazame runinga hizo bure badala yake warusha matangazo hayo wanawakatia huduma kama hawajalipwa.
Kuhusu Dstv na Azam kukata matangazo ya runinga za ndani baada ya kifurushi kwisha Dkt Abbas amesema suala hilo lipo Baraza la Ushindani hivyo wananchi wasubirie majibu na kwamba asingependa kulizungumzia kwa sasa.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA