JESHI LA POLISI ZANZIBAR LAAMUA KUJITATHMIN

Jeshi la Polisi Zanzibar,limeamua kujitathmini kwa lengo la kusahihisha kasoro watakazobaini ili kutoa huduma bora kwa jamii.
Mpango huo wa kujitathmini unafanyika kwa utaratibu wa kusikiliza maoni na ushauri kutoka kwa wananchi,wakilenga zaidi kujenga imani ya raia kwa jeshi hilo.
Utaratibu huo wa kujitathmini ulitangazwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kusini Unguja,Makarani Khamis Ahmed kuwa wameamua kufanya hivyo kwa lengo la kuliweka jeshi karibu na jamii na kufanya kazi pamoja ya kupambana na vitendo uhalifu.
Huu ni utaratibu mzuri wa kufanya mawasiliano na raia ambao unafaa kuendelezwa kwa maeneo yote ya visiwa vya Unguja na Pemba ambapo imeelezwa kuwa utaratibu huu utaondoa au kupunguza kwa kiasi kikubwa uadui au hofu iliyojengeka kati ya raia na polisi.
Aidha ni nafasi nzuri kwa maofisa wa Jeshi la Polisi kuwaelimisha raia na kuwaeleza dosari wanazoziona katika jamii katika kupambana na vitendo vya uhaifu na kuwatia hatiani wanaofanya vitendo hivyo.
Chanzo:Zanzibar24

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA