MAREKANI YAWAWEKEA VIKWAZO WATAALAMU WA MAKOMBORA KOREA KASKAZINI

Marekani imewawekea vikwazo maafisa wawili wa Korea Kaskazini akidai wamechangia kuundwa makombora ya nchi hiyo.



Haki miliki ya pichaREUTERS
Composite showing North Korean missile developers Ri Pyong-chol and Kim Jong-sik
Image captionKim Jong-sik na Ri Pyong-chol
Wizara ya fedha nchini Marekani iliwataja Kim Jong-sik na Ri Pyong-chol na kusema kuwa wote walikuwa viongozi wakuu katika mpango wa makombora ya masafa marefu wa Korea Kaskazini.
Baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa liliiwekea vikwazo vipya Korea Kaskazini siku ya Ijumaa kujibu majaribio yake ya makombora ya masafa marefu huku Korea Kaskazini ikisema kwa hatua hiyo ni kama ya vita.
Vikwazo hivyo vipya vya Marekani vitazuia shughuli zozote za wanaume hao wawili zinazofanywa nchini Marekani na hata kutwaliwa kwa mali yao zilizo nchini Marekani.
Wanaume hao wawili wanaonekana mara kwa mara wakiwa na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un wakiwa maeneo ya kuyafanyia majaribio makombora.
Mwaka huu nchi hiyo imefanya majaribio kadha ya makombora tofauti ambayo Korea Kaskazini inasema yanaweza kufika nchini Marekani.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA