WANANCHI MKOANI KATAVI WATAKIWA KUTOIOGOPA MAHAKAMA

Na.Issack Gerald
Wananchi Mkoani Katavi wametakiwa kutoiogopa mahakama kwa kuwa ipo kwa ajili ya kushughulikia mahitaji ya wananchi katika kupatikana na kwa haki zao.
Wito huo umetolewa na hakimu mwandamizi wa mahakama ya mwanzo mjini Mpanda Mh.David Daniel Mbembela kupitia kipindi cha kumekucha Tanzania kinachorushwa cha Mpanda Radio.
Aidha amewashauri wananchi kujenga tabia ya kufika katika mahakama kwa ajili ya kujifunza namna kesi zinavyoendeshwa mahakamani.
Wakati huo huo Mh.Mbembela amesema serikali imeleta baraza la ardhi la wilaya mkoani Katavi kwa ajili ya kusikiliza migogoro na kesi zinazohusu masuala ya ardhi ambapo awali wakazi wa Mkoa wa Katavi walikuwa wakipata huduma hiyo wilayani Sumbawanga Rukwa.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA