SERIKALI KUSHGHULIKIA HAKI ZA WALIMU

SERIKALI imesemna itaendelea kushughulikia haki za walimu pamoja na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu ikiwa ni pamoja na kushirikiana na chama cha walimu Tanzania ili walimu waendelee kufanya kazi katika mazingira rafiki kwa manufaa yao na taifa.

Kauli hiyo imetolewa leo  na Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Muhando kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga aliyetakiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa chama cha walimu Tanzania CWT wilayani Mpanda mkutano ambao umefanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari St.Mary’s Mpanda.
Awali akisoma taarifa ya chama kwa mgeni rasmi,katibu wa chama cha walimu Tanzania Wilayani Mpanda Wilison Masolwa,pamoja na mambo mengine amesema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo mifuko ya hifadhi ya jamii kukata na kuchelewesha malipo kwa walimu wastaafu suala ambalo wameiomba serikali kusimimia haki hizo ili kuhakikisha mwalimu anapata haki zake kwa wakati.
Kwa upande wake Mjumbe wa kamati ya utendaji wa CWT Taifa Bw.Hamis Ismail akizungumza kwa niaba ya Katibu mkuu wa Chama cha Walimu Taifa amesema pamoja na mafanikio ya kuanzisha benki ya mwalimu,kuanzisha ujenzi wa Ofisi za CWT Mkoa wa Katavi na kumtetea mwalimu,amewataka walimu kusimama na kutetea chama chao.
Wakati huo huo chama kimewapatia bati 40 walimu wawili wastaafu Aloyce Kapinga na Mrisho Kinanda  bati zenye thamani ya shilingi laki 680,000 pamoja na Shule ya Sekondari Mpanda Ndogo kupewa mifuko 5 ya simenti na 7 upande wa shule ya  Msingi Mpanda kama mchango wa ujenzi wa vyoo shuleni suala ambalo limepongezwa na waliopatiwa mchango huo.
Kwa mjibu wa utawala wa chama cha walimu Tanzania,Wilaya ya Mpanda inaundwa na Halmashauri mbili ambazo ni Mpanispaa ya Mpanda iliyopo wilayani Mpanda na Halmashauri ya wilaya ya Mpanda iliyopo wilayani Tanganyika ambapo katika mkutano huo uliokuwa umehudhuriwa na wanachama karibu 200 ulikuwa ukiwashirikisha pia wakuu wa wilaya,wakurugenzi,wawakilishi wa mifuko ya hifadhi,wataalamu wa idara katika Halmashauri na taasisi za kifedha.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA