ZIMAMOTO MKOANI KATAVI NYUMBA KWA NYUMBA KUEPUSHA HATARI-Septemba 6,2017

JESHI la zimamoto na uokoaji mkoani Katavi limesema linaanza oparesheni ya ukaguzi wa nyumba kwa nyumba  kubaini watu wenye tabia ya kuchimba vyoo au visima na kuacha bila kufukia  mashimo hayo  hali ambayo husababisha vifo vya watu wanapokuwa wametumbukia katika mashimo hayo.

Mkuu wa Ukaguzi wa Jeshi la Zima moto Koplo  Wilfred Ruhega amesema mwananchi atakayeshindwa kutii sheria bila shurti hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Ameongeza kuwa zoezi hilo la ukaguzi unaofanywa kwenye majengo pamoja na vyombo vya usafiri unaenda sambamba na tozo ambazo zipo tofauti kulingana na eneo husika.
Jeshi hilo linatoa kauli hiyo ikiwa ni kutoa mwongozo kwa wananchi ambao wamekuwa wakitoa taarifa kwa jeshi la polisi kwa kutokujua kwa kuwa majanga yote kama hayo yapo chini ya jeshi hili lililo chini ya Wizara ya Mambo ya ndani nchi.
Kwa upande wake Kopro Pastori Stanslaus Skwara Mthamini wa jeshi hilo mkoani katavi amesema viwango tofautitofauti vilivyoainishwa  vimepangwa kwa mujibu wa sheria hivyo ni vema wananchi kutii  sheria bila shuruti.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA