POLISI WAKAMATA PEMBE ZA NDOVU 666.


Polisi wa Tanzania wamekamata pembe 666 za ndovu zenye uzani wa tani 1.2 zenye thamani ya shilingi biloni 4.6 pesa za Tanzania sawa na dola milioni 1.2.
                           

Mkurugenzi wa idara ya jinai Bw.Diwani Athumani, amesema kuwa wageni wawili ni miongoni mwa watu 9 waliokamatwa katika operesheni hiyo.
Operesheni hiyo iliyohusisha maafisa wa polisi wa kimataifa kutoka Harare,Zimbabwe na Nairobi Kenya ilifanikiwa kupata genge la watu 43.
''operesheni ‘Usalama III’ ilianza juni tarehe 26 hadi tarehe 30 na ilihusisha maafisa kutoka mataifa 26 barani Afrika waliokuwa na jukumu la kupeleleza na kunasa genge lililohusika na uwindaji haramu''. alisema Athumani.
''Tulifanikiwa kuwanasa walanguzi hao pamoja na wawindaji haramu 256 pamoja na bidhaa zao zilizotengenezwa kwa pembe za ndovu''
Vile vile tulifaulu kukamata mihadarati kama vile heroine, bhangi, miraa mbali na silaha kali ikiwemo bunduki 12 na risasi 104'' alisema bwana Athumani.
''tutatoa bidhaa hizi zote kama sehemu ya ushahidi wa polisi mahakamani aliongezea kusema bw Athumani.
Athumani aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa washukiwa watafikishwa mahakamani karibuni.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA