AHUKUMIWA MIEZI 9 AKIDAIWA KUTOROKA AKIWA CHINI YA ULINZI WA JESHI LA POLISI WILAYANI MPANDA


Mahakama ya mwanzo mjini Mpanda imemhukumu mtu mmoja mkazi wa kata ya Misunkumilo kifungo cha miezi tisa jela kwa kosa la kutoroka akiwa chini ya ulinzi wa askari polisi.
                   

Akisoma hukumu hiyo,hakimu mwandamizi wa Mahakama hiyo Mh.David Mbembela amemtaja mtuhumiwa kuwa ni Mohamedi  Hamdany (24) ambaye alidaiwa kutenda kosa hilo Julai 7  mwaka huu usiku katika kituo cha polisi Mpanda mjini.
Aidha imedaiwa  kuwa  Bw.Hamdany alikuwa anakabiliwa na kesi nyingine ya  wizi wa pikipiki ambapo aliamua kutoroka akiogopa kupelekwa mahabusu ambapo alitoroka baada ya kuvua pingu aliyokuwa amefugwa mkononi na kukimbia kuelekea maeneo ya mtaa wa madukani .
Makosa ya watuhumiwa kutoroka chini ya ulinzi yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara wilayani Mpanda.
Kwa mjibu wa mahakama,  mtuhumiwa amefungwa kifungo hicho ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.
Katika hatua nyingine,Sanjari mtu mwingine anaefahamika kwa jina la Michael Damas (40) mkazi wa Tambukareli kata ya Mpanda Hotel amefikisshwa mahakamani kwa tuhuma ya kosa la  kuchoma moto nyumba  .
Akisoma shitaka hilo mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi CP Mtei amesema Bw.Damas alitenda kosa hilo Desemba 19 mwaka 2015 ambapo aliteketeza nyumba  na vitu vyote vilivyokuwa ndani vyenye thamani ya kiasi cha shilingi laki tano na elfu kumi na nne mali ya Anatalia Gulionkondwe.
Kwa upande wake mshitakiwa amekana kutenda kosa hilo na kesi hiyo imehairishwa hadi itakapo tajwa tena Julai 27 mwaka huu kwa ajili utetezi upande wa mshitakiwa

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA