WAKULIMA CHAMA CHA USHIRIKA CHA MSINGI MPANDA KATI WAHAKIKISHIWA MALIPO YA MAUZO YA TUMBAKU ASILIMIA 100.


Na.Issack Gerald-Katavi
Wakulima wa zao la tumbaku wa chama cha msingi cha ushirika Mpanda Kati Wilayani Mpanda Mkoani Katavi,wamehakikishiwa kulipwa asilimia 100 ya uuzaji wa zao hilo, kwa msimu wa mauzo ya 2015/2016.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa chama hicho Bw.Aman Rajabu wakati akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA Ofisini kwake kuhusu soko la zao hilo linalotarajia kuanza hivi karibuni.
Aidha,Bw. Rajabu amewataka wakulima wa tumbaku kuepuka watu wanaowashawishi kuuza zao hilo nje ya kampuni iliyosajiliwa ili kuepuka hasara inayoweza kuwapata.
Wakati huo huo,Meneja huyo amewataka wakulima wa zao la tumbaku wa chama cha ushirika Mpanda kati kuzingatia sera ya serikali ya upandaji miti ili kuepuka kuzuiwa kuendesha kilimo hicho kwa sababu ya kutopanda miti.
Chama cha msingi cha ushirika Mpanda Kati chenye wanachama wapatao 1600,kilisajiliwa mwaka 2014 na kwa mwaka 2015/2016 Jumla ya miti laki tisa na elfu sitini (960,000) imekwishapandwa na wanachama hao.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA