C.W.T KATAVI WAANDAMANA KWA MKURUGENZI MANISPAA KUDAI ZAIDI YA MILIONI 100 WANAZODAI KWA MIAKA 3 BILA MAJIBU



Na.Issack Gerald-Mpanda
CHAMA cha walimu mkoa wa katavi (CWT) kimefanya maandamano  katika ofisi za mkurugenzi wa manispaa ya mpanda kwa lengo la kushinikiza kulipwa madai yao.

Akizungumza kwa niaba ya wanachanma hao  mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Katavi Bw Gregory Mshota alisema  madai hayo ni sugu na yamedumu muda mrefu hivyo wanahitaji ufumbuzi wa haraka.
Amesema jumla ya  deni wanalo dai ni ya zaidi ya shilingi  milioni mia moja ambazo wamekuwa wakifuatilia kwa muda mrefu bila kuwa na majibu ya kulidhisha .
Kwa upande wa Katibu wa CWT Wilison Msolwa alisema sababu kubwa ambayo imewapelekea waandamane ni kikwazo cha muda mrefu kuhusoiana na madai yao.
Walimu ambao ni wanachama wa CWT wapatao 80 wanaotoka katika shule mbalimbali zilizopo Wilayani Mpanda wameshiriki maandamano hayo.
Kwa upande waken kaimu mkurugenzi wa manispaa ya mpanda Bi. Enelia Lutungulu mekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kuwaahidi wanachama hao  kushughulikia madai yao ndani ya miezi miwili kuanzia Machi 31.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA