ZAIDI YA BILIONI 26 NA BILIONI 43 ZAIDHINISHWA NA BALAZA LA MADIWANI NSIMBO KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO MWAKA WA FEDHA 2016/2017


Na.Agness Mnubi-Nsimbo.
HALMASHAURI ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi imeidhinisha kiasi cha shilingi billion 26,043,182,000 (Bilioni 26 milioni 43 na mia moja themanini na mbili elfu)  kwa ajili ya kutekeleza MIRADI mbalimbali iliyopangwa kufanyika katika Halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Fedha hizo zimeidhinishwa  na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo katika kikao cha bajeti ya mwaka wa fedha 206-2017 kilichofanyika leo katika ukumbi wa halmashauri hiyo.
Akisoma Bajeti hiyo mkuu wa idara ya mipango takwimu na ufuatiliaji Fredinand Filimbi amesema bajeti iliyotengwa imeandaliwa kwa  imezingatia sera na miongozo mbalimbali ya kitaifa.
Aidha bw. Filimbi amefafanua mchanganuo wa fedha hizo utatumika katika masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na mishahara,miradi ya maendeleo, na matumizi ya kawaida.
Amesema kiwango cha mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2016-2017 kimeongezeka kwa asilimia 12 na kutaja baadhi ya vyanzo vya ukusanyaji wa mapato hayo ikiwemo ushuru wa mifugo,magulio,nyama na vyombo vya uvuvi.
Aidha akifunga kikao hicho Mwenyekiti wa baraza la madiwani Rafael Kalinga ambaye ni diwani wa kata ya Machimboni amewataka madiwani na watumishi kuendelea kushirikiana ili kufikia malengo ya bajeti hiyo pamoja na kusimamia ukusanyaji wa mapato ,pia amewataka wakuu wa idara  kuhakikisha wanatekeleza miradi ya nyuma ambayo ilitengewa fedha.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA