MBUNGE JIMBO LA NKASI KUSINI ATAKA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA JIMBONI KWAKE,SERIKALI YAMJIBU


Na.Issack Gerald-Dodoma kuhusu (Rukwa)

SERIKALI imesema mwaka wa fedha 2015/2016 ilitenga Shillingi million 300 kwa ajili matengenezo na ujenzi wa Barabara ya Kitosi- Wampembe katika Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) ili kufanya Barabara hiyo iweze kupitika katika kipindi chote cha mwaka.
                                             

Serikali imetoa jibu hilo wakati wa swali la Mheshimiwa Mbunge Desdelius John Mipata Mbunge wa Nkasi Kusini ambaye ametaka kufahamu  mikakati ya serikali ya kilio cha  wananchi wanaopata shida kwa Barabara hizo kutopitika katika kipindi chote cha mwaka.
Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani amesema Serikali kupitia Wizara yake imesikia kilio cha wananchi wa Wilaya ya Nkasi na inaendelea kutoa fedha za matengenezo ya Barabara ya Kitosi-wampembe.
Ukarabati wa barabara ya Kitosi-Wampembe yenye urefu wa kilomita 67 na Barabara ya Nkana –kala yenye urefu wa kilometa 68 uko chini ya Mfuko wa Barabara ikisimamiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS) na Barabara zote ziko chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA