WAWILI MPANDA WAUAWA,WAUAJI WATOKOMEA KUSIKOJULIKANA NAO POLISI WASEMA HAPA KAZI TU


Na.Issack Gerald-MPANDA
Watu wawili wamekutwa wakiwa wameuawa na watu wasiojulikana Wilayani Mpanda Mkoani Katavi baada ya kukatwa na vitu vyenye ncha kali Januari Mosi Mwaka huu.

Mratibu wa Jeshi la Polisi Mkoani Katavi SSP Focas Malengo amesema,katika tukio la kwanza mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Tiho Robert (40) mkazi wa kitongoji cha Center John kijiji na kata ya Mwamkulu Wilayani Mpanda Mkoani Katavi,aliauawa majira ya saa tano za usiku.
Katika tukio hilo,marehemu alivamiwa na wauaji hao akiwa amelala nyumbani kwake baada ya kuvunja mlango na kuanza kumshambulia ambapo baada ya kutekeleza mauaji hayo walikimbia na kutokomea kusikojulikana.
SSP Malengo amesema,katika tukio lingine,mwanaume aliyekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25-30 aliuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kichwani na shingoni na watu wasiofahamika ambapo alikutwa katika maeneo ya mtaa na kata ya Nsemulwa amjira ya saa mbili asubuhi.
Hata hivyo chanzo cha mauji ya watu ahawa hakijajulikana na Jeshi la Polisi limesema Linaendelea na upelelezi ili kuwabaini wahusika na kuwafikisha katika vyombo vya kisheria.
Asante kwa kuendelea kuwa namii,endelea kuhabarika na P5 TANZANIA
Chanzo cha habari :Mratibu wa Jeshi la Polisi kny ya RPC Katavi

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA