JELA SIKU 14,KWA KUMCHANACHANA KWA NYEMBE MTOTO WAKE WA MIAKA 6


Na.Issack Gerald-MPANDA
Mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda imemhukumu Bi. Agnes George (30) mkazi wa Kawajense mjini Mpanda kwenda jela kwa siku kumi na nne,  baada ya kupatikana na hatia ya kumkatakata kwa nyembe nyuma ya viganja mtoto wake mwenye umri wa miaka sita, akimtuhumu kuiba fedha.

Akitoa ushahidi mahakama hapo, askari polisi wa kata, WP 3207 Copral Regina, ameiambia mahakama kuwa tukio hili lilitokea tarehe 25 Mwezi Novemba mwaka 2015 majira ya saa 3 asubuhi, alipigiwa simu na mwenyekiti wa mtaa wa Kawajense Bw. William Richard maarufu maka Jumapili akimtaarifu kuwa mtaani kwake kuna mama amekatakata mwanaye kwa wembe na alienda kwenye eneo la tukio la kumkuta mtuhumiwa akiwa amewekwa chini ya ulinzi na mama wneye nyumba, pamoja na akina mama wengine watano.
Amesema alimweka chini ya ulinzi na alishuhudia mtoto aliyejeruhiwa akiwa anatokwa na damu nyuma ya viganja vya mikono yake huku nyama nyeupe ikiwa inaonekana.
Mtuhumiwa alibebwa kwenye bajaji kwa ushirikiano na mwenyekiti wa mtaa, hadi kituo cha polisi mjini Mpanda kwa hatua zaidi za kisheria.
Copral Regina ameiambia mahakama hiyo kuwa, baada ya kugundua mtoto aliyejeruhiwa ana umri mdogo na hawezi kujieleza aliamua kumfungulia Agnes George shtaka la kujeruhi na hati ya matibabu ilitolewa na mtoto huyo alipelekwa hospitali na mshtakiwa baada ya kupewa dhamana.
Taratibu za kumfikisha mahakamani mtuhumiwa zilifanyika na hatimaye leo amefikishwa katika mahakama ya mwanzo mjini Mpanda ili kujibu mashtaka yanayomkabili.
Mshtakiwa amekiri kutenda kosa hilo mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Bw. David Mbembela na kwamba ushahidi uliotolewa ni wa kweli.
Hakimu  Mbembela amesema mshtakiwa ametiwa hatiani chini ya kifungu cha sheria namba 228 namba 2. Akijitetea mahakamani hapo Mshitakiwa Agnes George aliiomba mahakama imsamehe kwa kosa la kujeruhi mtoto wake na kwamba hatarudia tena hata kama mtoto huyo akirudia kuiba fedha atamfikisha polisi.
Akitoa hukumu Hakimu Mbembela amesema kulingana na kosa alilotenda mshtakiwa adhabu yake ni kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela, lakini kwa kuwa ni mkosaji wa mara ya kwanza ingawa mazingira yanaonesha alifanya kosa la unyanyasaji na hakupaswa kujichukulia sheria mkononi, hivyo mahakama imezingatia maslahi na umri wa mlalamikaji kwa kuwa bado anamtegemea mshtakiwa.
Mahakam hiyo imemhukumu kifungo cha siku 14 gerezani ili iwe fundisho kwa watu wenye tabia za unyanyasaji na kuagiza polisi ishirikiane na maafisa ustawi wa jamii kuhakikisha mhanga anapata uangalizi na pindi akitoka gerezani itabidi alipe gharama zitakazotumika kwa matunzo ya mtoto wake wakati akiwa gerezani. 
Asante kwa kuendelea kuwa namii,endelea kuhabarika na P5 TANZANI

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA