MLELE NAKO MAUJI KAMA MPANDA,MMOJA AUAWA,WAUAJI WATOKOMEA POLISI MSHIKEMSHIKE KUWASAKA WAUAJI


Na.Issack Mlele-Katavi
Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Chalya Kichosha(60) mkazi wa mkazi wa kijiji cha Ibindi alikutwa akiwa ameuawa na watu wasiojulikana kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu za kichwani na shingoni.

Mratibu wa Polisi Mkoani Katavi SSP Focas Malengo amesem akuwa tukio hilo limetokea Mnamo tarehe 02/01/2016 majira ya saa sita usiku katika kitongoji cha Ipilito Ibindi kata ya Ibindi Tarafa ya Nsimbo Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi.
SSP Malengo amesema,siku ya tukio,wauaji walifika nyumbani kwa marehemu majira ya usiku na kuvunja mlango kisha kuingia ndani na kisha kuanza kumshambulia  kwa kumkata sehemu za kichwani na shingoni hadi kupelekea umauti wake.
Chanzo cha mauaji hayo bado kujulikana. aidha, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wanakijiji cha ibindi linafanya msako ili kuweza kuwabaini wahusika wa tukio hilo.
Hata hivyo,Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi anatoa wito kwa wananchi kuacha mara moja tabia ya kujichukulia sheria mikononi kwa kutoa uhali wa binadamu wenzao badala yake wafate taratibu za kisheria katika kuwasilisha jambo au malalamiko dhidi yao katika vyombo vya kisheria ili kushughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi. Aidha, anaitaka jamii iendelee kushirikiana na Jeshi la Polisi kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili kufanikisha operesheni na misako ya kuwabaini na kuwakamata wote wa mauaji haya ili kuendelea kutokomeza vitendo vya namna hii ndani ya jamii
Asante kwa kuendelea kuwa namii,endelea kuhabarika na P5 TANZANIA
Chanzo cha habari :Ofisi ya mawasiliano ya Waziri

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA