WANAOGOMBANIA ARDHI NSIMBO WATAKIWA KUTOKA,ELIMU BURE BADO KUELEWEKA IPASAVYO KWA WANANCHI MKUU WA WILAYA YA MLELE ATOA NENO


Na.Agness Mnubi-Nsimbo.
WADAU wa Elimu katika halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wametakiwa kuelimisha wazazi na walezi juu ya Mfumo wa elimu bure.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Kanali Mstaafu Issa Suleiman Njiku katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika jana katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, mara baada ya madiwani wa halmashauri hiyo kuhoji juu ya Mfumo wa elimu bure.
Amefafanua kuwa ni wajibu wa Mkurugenzi kuitisha kikao cha wadau wa elimu ili kuwaelimisha wazazi na walezi  juu ya Mfumo wa elimu bure.
Aidha amesema taarifa juu ya  elimu bure zibandikwe kwenye mbao za matangazo, ili kurahisisha kusambaza elimu hiyo na kuwataka madiwani wa halmashauri ya Nsimbo kutoa taarifa za walimu wanaotoza ada na mahitaji mengine ya wanafunzi ambayo yanagharimiwa na serikali.
Wakati huo huo,idara ya Maliasili na Misitu katika halmashauri ya wilaya ya Nsimbo imeagizwa kutatua mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wa kata ya Urwila na kata ya Katumba, kuhusu kilimo katika eneo la Nzaga ambalo  ni chanzo cha mto.
Kanali Njiku ameongeza kuwa,wananchi wa Vijiji hivyo wanagombania kulima katika mpaka wa eneo la mto, kinyume cha sheria na kufafanua kuwa sheria inaelekeza shughuli za kibinadamu kuanza umbali wa mita 60 kutoka chanzo cha maji.
Kufuati hali hiyo, amewataka wananchi wanaoishi katika misitu na hifadhi ya serikali, kuhama na kuacha tabia ya kukata misitu na kuendesha shughuli yoyote katika hifadhi za serikali.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA