AMPA UJAUZITO DADA YAKE WA MIAKA 14 SUMBAWANGA POLISI WAMDAKA,IDARA YA ELIMU NAKO KALAMBO HARAKATI KWA KWENDA MBELE


Na.Issack Gerald-Sumbawanga
POLISI wilayani Sumbawanga Mkoani Rukwa inamshikilia mkazi wa kijiji cha Ulinji, Manispaa ya Sumbawanga mwenye umri wa miaka 28 kwa tuhuma za kumpa ujauzito dada yake mwenye umri wa miaka 14 anayesoma darasa la saba.

Inadaiwa kuwa mtuhumiwa ambaye amemtaliki mkewe, alirejea kuishi nyumbani kwa wazazi wake kijijini Ulinji miaka miwili iliyopita kabla ya kumpatia ujauzito mtoto huyo wa baba yake mkubwa.
Polisi imethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo na kwamba alikamatwa na Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ulinji, Manispaa ya Sumbawanga, Linus Mbutu.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ulinji, amesema mtuhumiwa amekamatwa juzi na askari wa Mgambo wa kijiji hicho akiwa amejificha kwa saa tatu porini akikwepa kukamatwa.
Katika hatua nyingine,idara ya elimu wilayani Kalambo  mkoani Rukwa jana imefanya kikao cha kujadili upungufu wa madawati uliopo wilayani humo.
Akizungumza na  P5 TANZANIA MEDIA sambamba na mpanda radio kwa njia ya simu afisa elimu vifaa na takwimu wa halmashauri ya wilaya ya Kalambo  Bi. Toba Mwihanga  ameziomba taasisi mbalimbali kutoa msaada ili kutatua changamoto hiyo.
Bi. Mwihanga amesema mwaka 2014 walipokea madawati 100 ambayo hayakukidhi mahitaji ya wanafunzi.
Aidha ameitaka jamii kuendelea kushiriki katika ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu na vyoo,huku akiwataka watendaji wa kata kuhamasisha jamii juu ya elimu bure , na kuiomba serikali kuongeza walimu katika mkoa huo.  

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA