WAKAZI KATAVI WATAKIWA KUWA MAKINI NA MVUA KUEPUKA MAFURIKO PIA IDARA ZA MAAFA KATIKA HALMSHAURI ZOTE ZAAGIZWA KUJIPANGA KIKAMILIFU


Na.Boniface Mpagape-Mpanda
MKUU wa Mkoa wa katavi Dk. Ibrahim Msengi amewataka wakazi wa mkoa huo,kuchukua tahadhari kutokana na uwezekano wa kuwepo kwa mafuriko kama ilivyotabiriwa na wataalam wa hali ya hewa.

Mkuu wa mkoa wa Katavi ametoa tahadhari hiyo wakati akizungumza na Mpanda radio ofisini kwake sambamba na P5 TANZANIA MEDIA.
Amesema wakazi wa mkoa wa Katavi wamekuwa wakijenga katika maeneo ambayo hayaruhusiwi kwa makazi na kuwataka wawe katika maeneo yasiyo hatarishi. 
Amewaagiza wakurugenzi, na wakuu wa wilaya zote mkoani Katavi   kwa kushirikiana na kamati zao za maafa kujiandaa kikamilifu kwa kutoa tahadhari kwa wananchi ili kukabiliana na maafa yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua za El-Nino.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA