RADI YAUA WAWILI YAJERUHI WATATU KATAVI


Na.Issack Gerald-Katavi

Watu wawili waliofahamika kwa majina ya Kupiwa Julius (28) na Lemmy Madirisha wote wakazi wa Mkazi wa Ilebura wamepigwa na radi na kufariki dunia papo hapo.

Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi Dhairi Kidavashari amesema kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya saa nane na nusu mchana katika kijiji cha Ilebura Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Mpanda.
Amesema kuwa,katika tukio hilo,watu watatu waliojeruhiwa wametajwa kuwa ni Tatu Gerald (28),Stela John (38) na Philbert Paschal wote wakazi wa kijiji cha Ilebura.
Aidha kamanda Kidavashari amesema,kabla ya tukio marehemu na majeruhi kwa pamoja walikuwa shambani wakilima ambapo wakati wakiendelea kulima mvua ilianza kunyesha ambapo wote waliamua kwenda chini ya mti kujikinga na mvua na ndipo radi ilipopiga na kupelekea madhara hayo.
Ameongeza kuwa baada ya tukio hilo majeruhi wote wamepelekwa katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda na wanaendelea na matibabu huku miili ya marehemu ikiwa imekabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya mazishi.
Hata hivyo,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi anawatahadharisha wananchi wote kuwa makini katika kipindi hiki cha masika pindi mvua zinaponyesha kwa kujihifadhi maeneo salama ilikuepukana na madhara kama haya ambayo huadhiri ustawi wa afya na uhai wa watu.
P5 TANZANIA MEDIA inatoa pole kwa ndugu jamaa na marafiki waliofikwa na msiba na mungu awaponye majeruhi warudi katika hali yao ya afya kama kawaida.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA