WANANCHI KATAVI WAIOMBA SERIKALI YA AWAMU YA TANO CHINI YA MAGUFULI KUUNDA MAHAKAMA YA KIFAMILIA


Na.Agness Mnubi-MPANDA.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya tano Ya Dk. John Pombe Maghufuli  imeombwa kuunda Mahakama ya Kifamilia itakayojihusisha na  kushughulikia vitendo vya ukatili na unyayasaji wa kijinsia.
Ombi hilo limetolewa na Mwenyekiti wa Asasi ya Kiraia inayofahamika kama Faraja na  Urafiki kwa Wanandoa na Ushauri kwa Vijana(FUNUVI )  Bi.Neema Kidima Mkoani Katavi,wakati akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA na mpanda redio juu ya mikakati ya kutokomeza vitendo vya ukatili katika familia,jamii na Taifa kiujmla kwa mwaka 2016.
Amependekeza kuwa mahakama hiyo iendeshwe  na wasimamizi wa kisheria na iwapo kesi ikishindikana mahakamani hapo  ipelekwe katika ngazi za juu za kisheria.
Bi. Kidima amefafanua kuwa kuundwa kwa Mahakama ya kifamilia, vitendo vya ukatili na unyanayasaji wa kijinsia vinavyojitokeza vitashughulikiwa kwa ukaribu zaidi kuliko ilivyo sasa ambapo idara inayoshughulika na masuala ya ukatiri kwa watoto huchelewa kuyafanyia maamuzi kutokana na kuwa wanashuhulikia masuala mengine ambayo yanakuwa yameletwa katika ofisi hizo.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA