BREAKING NEWS : MTOTO (16) ALALA NJE TANGU UTOTONI CHANZO WAZAZI KUMFUKUZA NYUMBANI,TAASISI ZA KUPINGA UNYANYASAJI ZAINGILIA KATI.


Na.Agness Mnubi-MPANDA.
MTOTO anayefahamika kwa jina la Adamu Ramadhan mkazi wa Manispaa ya Mpanda, yuko katika hatari ya kuathirika kisaikolojia kutokana na vitendo vya kikatili.

Asasi ya FUNUVI inayohusika na faraja kwa Wanandoa na Vijana mkoani Katavi katika barua yake yenye kumb.Na FUNUVI/MPD/MND/1/015 imekiri kupokea malalamiko ya kijana huyo.
Kijana huyo (takribani miaka 16) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Kashaulili amefukuzwa nyumbani na wazazi wake jana na kusababisha aishi maisha ya hatari.
Akihojiwa na P5 TANZANIA MEDIA sanjari na Mpanda Radio ,mtoto huyo amekiri kufanyiwa ukatiri na ikiwemo kupigwa na mama yake wa kambo.
Juhudi za kuwapata wazazi na maafisa wa ustawi wa jamii na jeshi la polisi kitengo cha dawati la jinsia na watoto zinaendelea.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA