KAMANDA WA POLISI MWANZA ATOA TAARIFA YA ASKARI KUMUUA KWA RISASI ASKARI MWENZAKE


NA.Mwandisi wetu-MWANZA

Askari mmoja  wa jeshi la Polisi mkoani Mwanza  jana amefyatua risasi na kumuua asikari mwenzake kisha nayeye kujipiga risasi na kufariki dunia katika lindo la benki ya posita jijini mwanza huku chanzo cha tukio hilo kikiwa hakija julikana.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza  kamishina msaidizi wa Polisi Justus Kamugisha amethibitisha kutokea kwa tukio na kwamba limetokea majira ya saa nane na nusu mchana katika lindo la Banki ya Posta tawi la Pamba  jijini Mwanza.
 Kamanda Kamugisha amewataja askari hao kuwa ni Konstebo H 852 Daud Masunga Elisha aliyempiga risasi Pc Petro Simoni Matiko H5950 eneo la begani na baadae Pc Masunga kujipiga risasi eneo la paji la uso na kufariki pao hapo, wote ni askari wa wilaya ya Nyamagana
Aidha Kamanda Kamgisha amesema jeshi la Polisi lina endelea na uchunguzi juu ya tukio hilo  ili kubaini chanzo cha mauaji hayo.


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA