BODABODA MPANDA WAZUNGUMZIA MIUNDOMBINU MIBOVU YA BARABARA INAVYOATHIRI UCHUMI WAO


Na.Issack Gerald-MPANDA
Miundombinu mibovu ya barabara hususani kipindi hiki cha masika imeathiri uchumi wa waendesha pikipiki katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Matavi.

Hayo yamebainishwa na waendesha pikipiki hao wakati wakizungumza na P5 TANZANIA MEDIA na mpanda redio ambapo wamesema kuwa barabara nyingi hasa vijijini hazipitiki kutokana na mabonde hali inayowafanya kufanya shughuli hiyo  mjini pekee.
Katika hatua nyingine madereva hao wamesema,katika kuzua ajali za barabarani hasa kipindi hiki cha msimu wa sikukuu wamejipanga kuendesha pikipiki kwa umakini mkubwa kutokana ongezeko la vyombo vingi vya moto barabarani.
Takwimu zinaonyesha kuwa katika kipindi cha sikukuu matukio ya ajali huongezeka kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo madereva kuendesha kwa mwendokasi pamoja na ulevi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA