AFARIKI DUNIA BAADA YA KUFUKIWA NA KIFUSI AKICHIMBA DHAHABU NSIMBO KATAVI


Na.Issack Gerald-Mpanda
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina Mateo Robert(33) mchimbaji mdogo mkazi wa Mbeya-Songwe,amefariki dunia baada ya kuangukiwa na lundo la udongo akiwa kwenye shimo (LONG BASE) wakati akichimba madini ya dhahabu.

 Kamanda wa polisi Mkoani Katavi Dhahiri Kidavashari amesema kuwa tukio hilo limetokea Mnamo tarehe 23.12.2015 majira ya saa 09:00 kwenye Machimbo ya dhahabu ya wachimbaji wadogo ya Nsimbo yaliyopo kijiji cha Katuma, Kata ya Katuma, Tarafa ya Mwese Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi.
Kamanda amesema kuwa marehemu akiwa na wenzake wawili ambao ni Edson David Akiba(25 mchimbaji Mkazi wa Kigoma pamoja na Tungu Thomas(30) mchimbaji Mkazi wa mkoa wa Shinyanga walielekea mgodini hapo kufanya shughuli zao za uchimbaji kama ilivyo kawaida yao ambapo wakati wa uchimbaji huo marehemu na mwenzake aitwaye Tungu Thomas walikuwa wameingia shimoni na nje shimo walimuacha mwenzao ambaye ni Edson David Akiba ambapo baada ya muda mfupi kilisikika kishindo kutoka ndani ya shimo.
Kutokana na hali hiyo  Edson David alijaribu kuwaita wenzake waliokuwa shimoni hawakuitika ndipo harakati za kuwasaidia zilipofanyika kwa kuwaita wachimbaji wengine wa maeneo jirani ambapo baada ya kuingia marehemu alikutwa kafunikwa na udongo akiwa tayari kafariki dunia huku mwenzake Tungu Thomas akiwa amejeruhiwa kichwani.
Aidha Kamanda Kidavashari amesema,kwa mujibu wa uchunguzi wa kitabibu kifo cha marehemu kilitokana na majeraha aliyoyapata kichwani (HEAD INJURY) na mwili wake ulikabidhiwa kwa ndugu zake kuendelea na taratibu zingine za mazishi, huku Tungu Thomas  akipatiwa matibabu katika hospitali ya Katuma na kuruhusiwa kwenda kujiuguzia nyumbani.
Hata hivyo si mara ya kwanza matukio kama haya kutokea ikizingatiwa kuwa hivi karibuni wachimbaji wadogo walifukiwa katika mgodi wa Nyangalata uliopo Wilayani Kahama.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA