WAZAZI,WALEZI KATAVI WAASWA KUWAPELEKA VIJANA WAO KATIKA VYUO KUPATA SOKO LA AJIRA


Na.Issack Gerald-MPANDA
WAZAZI na walezi mkoani katavi wameshauriwa kuwapeleka vijana wao katika vyuo mbalimbali vya mafunzo ya ufundi stadi VETA  ili waweze kupata elimu itakayowasaidia kuingia katika soko la ajira ikiwa pamoja na kujiajiri wenyewe pindi wamalizapo masomo yao.

Ushauri huo umetolewa na na mgeni rasmi  katika mahafali ya 26 ya kuwaaga wafunzi  wa chuo cha VETA Mpanda Bw. Sebastian Kapufi ambaye pia ni mbunge wa mpanda  mjini.
Amesema wazazi wa mkoa wa katavi wanapaswa kuitambua na kuitumia fursa iliyopo ya kuwa na chuo cha ufundi karibu yao kwa kuwasomesha vijana wao.
Aidha katika mahafali hayo Bw. Kapufi ametoa shilingi milioni moja kama zawadi ya wahitimu waliomaliza masomo yao katika fani mbalimbali chuoni hapo.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA