WATENDAJI WALIOGOMA KUHUDHURIA KIKAO CHA MKURUGENZI WILAYA YA MPANDA KUKABILIWA NA ADHABU


Na.Issack Gerald-MPANDA
HALMASHAURI ya wilaya ya Mpanda imeagiza kuchukuliwa hatua kwa watendaji wa kata na vijiji walioshindwa kuhudhuria kikao cha kazi kilichoitishwa na mkurugenzi bila taarifa.
Agizo hilo limetolewa jana na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Bw. Estom Chang’a katika kikao cha maelekezo ya utekelezaji wa kazi za kutatua kero za wananchi katika maeneo yao.
Kikao hicho cha kazi kimewashirikisha watendaji wa kata mbali mbali wakiwemo maafisa maendeleo ya jamii katika ngazi ya vijiji kutoka kata zote za halmashauri ya wilaya ya Mpanda. 

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA