KATA YA SITALIKE KUKUSANYA MAPATO KUTOKA MIGODINI NA HIFADHINI

Na.Issack Gerald-NSIMBO
UONGOZI wa Kata ya Sitalike wilayani Nsimbo mkoani Katavi, unatarajia kukusanya mapato kutoka kwa wawekezaji wa migodi pamoja na hifadhi ya taifa ili kuchangia maendeleo ya kata hiyo.

Diwani mteule wa Kata hiyo Bw. Adam Galamila ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Mpanda redio, mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mtisi.
Bw. Galamila amesema katika kata ya Sitalike kuna migodi mingi ya wawekezaji pamoja na hifadhi ya taifa, ambayo kama michango yao itatumika vizuri kata hiyo itapiga hatua kimaendeleo.
Aidha, amesema mgogoro wa ardhi uliopo baina ya wakazi wa kata hiyo na hifadhi ya taifa unaendelea kutafutiwa ufumbuzi ili wakazi wa kata hiyo waweze kufanya shughuli za kilimo.


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA