HALMASSHAURI YA MJI NJOMBE YAWAONYA WALIMU WAKUU WATAKAOFELISHA WANAFUNZI


Na.Mwandishi wetu-NJOMBE

Halmashauri ya mji wa njombe imesema itaendelea kutoa adhabu za kuwa vua vyeo walimu wakuu ambao shule zao zinafelisha wananfunzi kuufikia wastani waliojiwekea ili kukuhakikisha halmashauri hiyo inangara kielimu kwa kufikia ufaulu wa juu.

Afisa elimu msingi wa halmashauri hiyo zegeli shengeli amesema kuwa kwa mitihani ya darasa la saba mwaka huu halmashauri hiyo imeongeza ufaulu amapo kwa mwaka jana zaidi ya shule 15 zililikua chini ya ufaulu lakini kwa sasa shule 5 pekee zimeshindwa kuvuka ufaulu unaotakiwa
Amesema kuwa miongoni mwa adhabu zinazotolewa kwa wakuu ambao wameshindwa kufaulisha ni pamoja na kuvuliwa vyeo na kuhamishwa ili wajifunze na kwama kufanya hivyo kumezaa matunda kwa shule nyingi kufanya vizuri
Shule ya msingi Itipula ni miongoni mwa shule zilizofanya vibaya katika mtihani wa darasa la saba kwa kushika nafasi ya mwisho kati ya shule 78 ambapo afisa elimu amebainisha kuwa miongoni mwa sababu za kuanguka kielimu ni kukosekana kwa ushirikiano baina ya walimu na kamati na wazazi
Kwa upande wake mkuu wa shule ya itipula Ogorino ngoitanile amekiambia kituo hiki kuwa tatizo la kufeli kwa wanafunzi shuleni hapo linatokana na wazazi waliowengi kuwa na watoto wengi ambao wanashindwa kumudu kuwasomesha hivyo kuwa shawishi kufanya vibaya mitihani ili kukwepa majukumu ya kuwasomesha wakifaulu
Wazazi wa wananfunzi shule ya msingi itipula wamekiri kuwa chanzo cha wanafunzi kufeli mitihani kwa madai kuwa kumekuwa na adhi yao huwafuata walimu na kuwatishia pindi wanapo toa adhabu kwa watoto wanao feli masomo na hivyo kupelekea walimu kukata tamaa ya kufeli

Pia wameshauri serikali kuwachukulia hatua kali wazazi wenye tabia ya kuwatishia wazazi ili kuleta maendeleo ya taaluma katika shule yao


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA