CWT KATAVI KUDAI ZAIDI YA MIL..379


Na.Issack Gerald-KATAVI
HALMASHAURI Za Wilaya ya Mpanda,Nsimbo na Manispaa ya Mpanda zimetakiwa kulipa madeni yanayodaiwa na walimu wa shule za Msingi na Sekondari Mkoani hapa.
Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa chama cha walimu Tanzania CWT Mkoa Bwana John Gregory Mshota amesema halmashauri hizo zinadaiwa na walimu zaidi ya shilingi Milioni 379 kutokana na malimbikizo ya malipo mbalimbali.
Katika hatua nyingine Bwana Mshota amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi Kuingilia Kati suala la Upotevu wa hati za Mshara wa walimu  Waliokuwa halmashauri ya Mji Mpanda Kabla ya kuwa manispaa kwa  Mwezi Augost 2008 ,Kama alivyoahidi Mwezi February mwaka huu, Katika kikao cha pamoja na walimu wa shule za Msingi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA