WAKAZI WALALAMIKA KITUO CHA AFYA KUKOSA CHUMBA CHA KUHIFAHIDHIA MAITI


WAKAZI wa kata ya mtowisa wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa wamelalamikia kitendo cha kituo cha afya Mtowisa ambacho ni kikongwe kwa zaidi ya miaka 20 kutokuwa na chumba cha kuhifadhia maiti kitendo kinachosababisha wagonjwa kukaa na maiti muda mrefu wodini baada ya mtu kufariki.
Wakizungumza mbele ya mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo alipokuwa katika ziara yake ya kikazi na kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji hicho. 
Wakazi hao walimweleza mkuu huyo wa mkoa kuwa wagonjwa wanalazimika  kulala na miili ya marehumu wardini  huku wakisubiri ndugu wa marehamu kufika na kuchukua miiili hiyo kwa maziko na wakati mwingine maziko ya baadhi ya watu yamekuwa yakifanyika haraka bila kusubiri ndugu wa karibu na marehemu hao kutokana na kuzikwa mapema kwa kuhofia kuharibika kutokana na  kukosekana chumba cha kuhifadhia maiti.
Mmoja wa wakazi hao  Christina Mponji alisema kuwa iwapo kifo kikimfika mgonjwa aliyekuwa amelazwa jirani na kitanda chako hali inayosababisha kupatwa na hofu jambo linalosababisha kutoroka hospitali kabla huduma za matibabu hazijakamilika.
Naye Msafiri Malema alisema  kukosekana kwa chumba cha kuhifadhia maiti jambo hilo limetokana na uongozi wa kata kutokuwa na hamasa ya kuwahamasiasha wananchi kujitokeza katika nguvukazi ya ujenzi wa chumba hicho  kitendo ambacho kingeondowa changamoto hiyo.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa huo  Wangabo aliwataka wakazi wa kata hiyo kuanza mara moja  nguvu kazi kwaajili ya ujenzi wa huku akiwaahidi kutoa bati  wa watakapokuwa wamekamilisha ujenzi wa chumba hicho cha akuhifadhia maiti
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA